Loma Linda University

Mpango wa Usambazaji wa Diapu wa Mitaa ya San Bernardino Wafikia Hatua ya Diapu Milioni 1

Juhudi za kuwafikia jamii, zinazoongozwa na Loma Linda University Health kwa ushirikiano na mashirika mbalimbali, zimeathiri wengi wanaokabiliana na mfumuko wa bei na changamoto za kifedha.

Picha: LLU

Picha: LLU

Mpango wa kusambaza nepi au diapu mara mbili kwa mwezi huko San Bernardino, California, hivi majuzi ulisherehekea hatua muhimu ya nepi milioni 1 zilizosambazwa tangu programu hiyo ilipozinduliwa Agosti 2022. Viongozi wanakadiria kuwa mpango huo umewaokoa wakaazi wa eneo hilo dollaza markani $250,000 wakati ambao, kwa watu wengi, imekuwa ngumu kifedha kutokana na kupanda kwa mfumuko wa bei.

Mpango huo unaratibiwa na Chuo Kikuu cha Loma Linda Health (LLUH) kwa ushirikiano na vikundi kadhaa vya jamii, ikiwa ni pamoja na Ushirikiano wa Utekelezaji wa Jamii (Community Action Partnership) ya Kaunti ya San Bernardino, Wilaya ya Shule ya San Bernardino ya Jiji la San Bernardino (San Bernardino City Unified School District), na Kituo cha Elimu cha El Sol Neighborhood kupitia Mpango wa Wafanyakazi wa Afya na Elimu ya Jamii (Community Health & Education Worker, CHEW).

Ushirikiano wa Utekelezaji wa Jamii (Community Action Partnership) ya Kaunti ya San Bernardino ilibainisha hitaji la nepi, ambazo zinaweza kuhitaji hadi asilimia 20 ya mapato ya wakazi wa eneo hilo, ambao wengi wao hufanya kazi za ujira mdogo. Kikundi cha ushirika cha kaunti kilikaribia LLUH kwa usaidizi wa usambazaji kwa sababu ya uzoefu wake wa kuratibu usambazaji wa chakula wakati wa janga la COVID-19.

Mpango huo unafanya kazi nje ya sehemu ya maegesho ya shule ya msingi na kusambaza diapers karibu 80,000 kwa mwezi, viongozi wanasema. Nepi hutolewa na serikali kupitia mpango wa ushirikiano wa jamii wa kaunti. Wafanyikazi wa ghala la LLUH hufanya kazi ya kuhifadhi na kutoa diapers kwa kila tukio la usambazaji.

"Tunataka kusherehekea familia zinazokuja, kwa hivyo tuko nje kila wakati, mvua au jua," alisema Cristie Granillo, MEd, MS, wa Taasisi ya Afya ya Chuo Kikuu cha Loma Linda kwa Ushirikiano wa Jamii na meneja wa programu ya CHEW.

Mahusiano thabiti ya jamii yamekuzwa kupitia mpango huu, na kuruhusu timu kufanya kazi ili kuziba mapengo ya usawa wa afya kwa kuzambaza rasilimali muhimu kama vile huduma za matibabu na usajili wa shule, elimu ya kujisaidia chooni, na ufahamu wa programu zingine.

Madereva hupanga magari yao wakingoja usaidizi na mara nyingi hupewa vitu vya ziada au marejeleo kwa huduma zingine, kama vile shule ya mapema kwa watoto wao au ushauri wa lishe ya familia. Watu wa kujitolea pia husambaza masanduku 600 ya chakula kila mwezi.

Tukio hilo limesaidia watu kama Monique Walter, ambaye ana watoto tisa na hivi karibuni ameona kodi ya nyumba yake ya kila mwezi ikiongezeka kwa takriban asilimia 30. "Ni vizuri sana kupokea hizi kwa sababu nepi ni ghali sana sasa," Walter alisema kwenye mstari huku akihudumiwa na mfanyakazi wa kujitolea.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Loma Linda pia hushiriki katika hafla hiyo, kama watu wa kujitolea au kama hitaji la vitendo kwa programu yao ya masomo. Wengi wanatoka Shule ya Tiba, Shule ya Afya ya Umma, Shule ya Madaktari wa Meno, au Shule ya Afya ya Tabia.

Picha:LLU

The original version of this story was posted on the Loma Linda University Health website.

Makala Husiani