South Pacific Division

Nyanya Shujaa Aokoa Watu 17 katika Maporomoko ya ardhi ya Papua New Guinea

Janga hilo limewahamisha maelfu ya watu na inakadiriwa kuwa watu 670 wamefariki, huku 2000 wakiaminika kuzikwa wakiwa hai.

Maporomoko ya ardhi yalisababisha "uharibifu mkubwa" katika kijiji cha Yambali katika mkoa wa Enga.

Maporomoko ya ardhi yalisababisha "uharibifu mkubwa" katika kijiji cha Yambali katika mkoa wa Enga.

[Picha: Adventist Record]

Zaidi ya watu 7000 waliathiriwa na maporomoko ya ardhi yaliyokuwa na madhara makubwa huko Mulitaka, Mkoa wa Enga, Papua New Guinea (PNG), siku ya Ijumaa, Mei 24, mwaka wa 2024. Janga hilo, lililotokea karibu saa tisa alfajiri, liliwahamisha maelfu ya watu na inakadiriwa kuwa watu 670 walipoteza maisha, huku 2000 wakiaminika kuzikwa wakiwa hai.

Luke Nathan, raisi wa Misheni ya Western Highlands, aliripoti kwamba washiriki 70 wa kanisa la Waadventista walikuwa wameathirika, lakini hakuna maisha ya Mwadventista yaliyopotea. Kanisa la eneo hilo lilipata uharibifu wa sehemu, huku kutokuwa na utulivu katika eneo hilo kunatishia hatari za baadaye.

Timu ya kukabiliana na majanga ya ADRA inasafiri hadi eneo lililoathiriwa wiki hii. Timu hiyo itatekeleza mpango wa kukabiliana, unaojumuisha kununua na kusambaza bidhaa za msaada kama vile chakula, vifaa vya usafi na vitanda.

Wanaojiunga na timu ya ADRA ni Nathan, Malaki Yani, rais wa Misheni ya Muungano wa PNG, na zaidi ya washiriki 50 wa kanisa ambao watafanya kazi pamoja na ADRA wakati wa usambazaji. Timu pia itafanya tathmini ya mahitaji.

Nyanya Mwadventista Shujaa

Mshiriki wa kanisa mwenye umri wa miaka 70 ambaye alinaswa kwenye maporomoko hayo aliokolewa baada ya kuokoa maisha ya watu 17—watu wazima saba na watoto 10, kulingana na Papua New Guinea Post-Courier. Kion Kopal Diai, ambaye alikuwa amelala kwenye nyumba ya kulala wageni inayomilikiwa na mwanawe, aliamshwa na sauti ya kunguruma. Baada ya kuwatahadharisha wageni waliotoroka, Diai alirudi chumbani kwake wakati nyumba ya kulala wageni iliposombwa na maporomoko ya ardhi.

"Nyumba ya kulala wageni ilizikwa kabisa na mama Kion ndani," iliripoti Post-Courier. Bi Diai aliokolewa na mamlaka katika kile makala inachoeleza kama "kutoroka kwa kimiujiza".

Mjukuu wake Desmond Kopen alishiriki hadithi na gazeti, akisema nyanya yake ni "shujaa wa maombi katika kanisa la mtaa huo la Waadventista".Nyanya

Makala asili ilichapishwa kwenye tovuti ya habari ya Divisheni ya Pasifiki Kusini, Adventist Record.