Kijana Mwaadventista Kuonyesha Kazi Zake kwenye Louvre

South American Division

Kijana Mwaadventista Kuonyesha Kazi Zake kwenye Louvre

Sophia Helena ana miaka 10 na atakuwa na maonyesho kwenye Louvre Carousel mwezi wa Oktoba mwaka huu.

Hadithi ya Sophia Helena Moreira de Oliveira ilianzia katika chuo cha Colégio Adventista de Jacarepaguá, alipokuwa na umri wa miaka sita alionyesha ujuzi wa kisanii ambao ulikuwa tofauti na ule wa watoto wa umri wake. Mwalimu wake wakati huo aliwasiliana na mama yake na kumwomba amkubali aweze kuwekeza katika kibaji hiki. Jambo ambalo hawakulifikiria ni kwamba miaka mitano baadaye, Sophia angepata fursa ya kuonyesha michoro yake kwenye jumba la makumbusho la Louvre, nchini Ufaransa, lililotembelewa na watu zaidi ulimwenguni.

Akiwa na umri wa miaka 10 tu, Sophia Helena alichaguliwa katika shindano la kimataifa na kazi zake mbili zitaonyeshwa kwenye Louvre Carousel, nafasi iliyojitolea kwa vipaji vipya. Maonyesho hayo yatafanyika Oktoba 2024.

Madureira ni kitongoji cha kitamaduni katika vitongoji vya Rio de Janeiro na ni sehemu ya eneo la Associação Rio Sul (ARS), makao makuu ya kiutawala ya Kanisa la Waadventista Wasabato katika eneo la kati na kusini mwa Rio de Janeiro.

Rais wa Yunioni ya Rio Sul, mchungaji Geovane Souza, alishangazwa na talanta ya msichana huyo mdogo. "Tunapoona watoto wakivumbua talanta zao na kumpa Yesu, tunajisikia furaha sana na hali ya utume imekamilika", anasema Souza, ambaye anaanzisha mafanikio ya Sophia.

Kazi ya Msanii huyu Mtoto

Wanasesere (dolls) au michezo ya kielektroniki havimvutii Sophia inapokuja suala la kujiburudisha au kufurahia. Anapenda sana kutumia wakati wake mwingi kuchora au kupaka rangi michoro. Kipaji chake kiligunduliwa mapema na mwalimu wake wa Pre II, ambaye alivutia macho ya mama yake, Daniele Moreira. "Mwalimu wake alikuwa msingi katika mchakato huu. Yeye ndiye aliyenishauri kuwekeza katika kibaji cha Sophia", anaelezea, akifurahia binti yake kwamba ataishi uzoefu ambao utamtia alama kwa maisha yake yote.

Kwa Sophia, tukio hili ni mwanzo tu wa mafanikio zaidi ambayo Mungu anayo kwa maisha yake. Baada ya kupokea habari kwamba alikuwa amepita uteuzi huo, alihisi mchanganyiko wa hisia. "Wakati huo huo nikiwa na wasiwasi na hofu, nilijiamini. Ninajaribu kuacha wasiwasi wote kuhusu siku zijazo mikononi mwa Mungu, kwa sababu najua kwamba ataongoza maisha yangu", anaripoti msanii huyo.

Akiwa na umri wa miaka 7, alimwomba mama yake kununua kanvasi, na tangu wakati huo, alijigundua katika ulimwengu wa uchoraji. Mojawapo ya michoro yake ya kwanza ilikuwa sura ya Yesu, ambayo ilionyeshwa katika maonyesho yaliyoendeshwa na Klabu ya Adventurers, programu kwa ajili ya watoto wa Kanisa la Waadventista wa Sabato ambayo inajumuisha shughuli za burudani, elimu, na kiroho.

Akiwa na umri wa miaka 9, alianza masomo ya uchoraji katika studio maalum na akapata mawasiliano yake ya kwanza na uchoraji wa kitaalamu ukitumia rangi ya akriliki. "Siku ya kwanza nilianza uchoraji, uchoraji wangu wa kwanza, uliitwa 'Nyumba ya Friburgo'. Mwalimu wangu na wanafunzi wengine walishangazwa na kipaji changu," anasema.

Hivi sasa, Sophia mara nyingi huchora mandhari, wanyama na sanaa ya kufikirika na rangi ya akriliki. Kulingana naye, analenga kuhamasisha mtazamaji kuwa na "furaha, mawazo chanya, kupendezwa na sanaa na utamaduni", anaelezea jinsi anapenda kuathiri watu na sanaa yake. Baadhi ya kazi zake tayari zimeonyeshwa katika Jumba la sanaa la Usanifu na huko Aliança Francesa, huko Fribourg.

Kipaji cha Kiungu

Akiwa amelelewa katika nyumba ya Mwaadventista, Sophia amekuwa akishiriki katika shughuli za kanisa na, kwa kibaji chake, anaweza kutafuta njia tofauti za kuonyesha upendo wa Yesu. "Popote nilipo, ninaweza kumshuhudia Yesu kwa maneno yangu, matendo yangu, na kumwacha Mungu kwanza maishani mwangu", aeleza.

Kwa profesa Robledo Moraes, mkurugenzi wa mtandao wa Elimu ya Waadventista katika kituo cha kusini cha Rio de Janeiro, Elimu ya Waadventista imejitolea kuwaelekeza wanafunzi kugundua zawadi yao na kuitumia kwa njia ya heshima.

"Mwaka wa 2018, nilipata fursa ya kukutana na Dkt. Cristina Delou. Yeye ni mmoja wa mamlaka kuu nchini Brazil linapokuja suala la vipaji vya juu. Alitaja wakati huo kwamba kuna uwezekano wa kuwa na wanafunzi wenye vipaji vya juu katika shule zote. Baadhi yao, kwa kiwango kikubwa, wengine kwa asilimia ndogo, lakini wapo," anaeleza Robledo.

Anasisitiza kwamba "kuwatafuta wanafunzi hawa na kuwapa njia ya kujiendeleza ni changamoto na Elimu ya Waadventista imejitolea kwa hili."

The original article was published on the South American Division Portuguese news site.