• Lugha
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • Kuhusu ANN
    • Mahitaji ya utoaji
    • Mwongozo wa Mtindo
  • World
  • Amerika
  • Asia
  • Ulaya
  • Afrika
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

ANN na Adventist.news ni njia rasmi za habari za kanisa la Waadventista Wasabato.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Matumizi ya Alama ya Biashara na Nembo
  • Notisi ya Kisheria
  • Sera ya faragha
© 2026 Copyright ©2024, General Conference of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike, 20904 Silver Spring, MD USA 301-680-6000
  • World
  • Amerika
  • Asia
  • Ulaya
  • Afrika
  • Oceania
  • Vyombo vya habari
  • Lugha
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • Kuhusu ANN
    • Mahitaji ya utoaji
    • Mwongozo wa Mtindo
Seventh Day Adventist Logo

ANN na Adventist.news ni njia rasmi za habari za kanisa la Waadventista Wasabato.

Waadventista Wasabato wamejitolea kuwasaidia watu kuielewa Biblia kupata uhuru.

Jifunze zaidi

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

Trans-European Division

Wajitolea wa Amerika ya Kilatini Wahudumu Katika Dirisha la Baada ya Ukristo la Uswidi

Wamisionari sita vijana wanapeleka huduma inayolenga imani na afya katika mojawapo ya maeneo magumu zaidi ya kimisheni duniani kupitia LifeStyleTV.

14 Agosti 2025

Uswidi

Tor Tjeransen, KOnferensi ya Yunioni ya Norwe
Kutoka kushoto kwenda kulia: Natalia Cárdenas kutoka Guatemala, Cintia Stoletniy kutoka Argentina, Vianka Aranky kutoka Honduras na Delfina Dupont kutoka Argentina, wakihudumu kama wajitolea katika LifeStyleTV na LifeStyleSTAY.

Kutoka kushoto kwenda kulia: Natalia Cárdenas kutoka Guatemala, Cintia Stoletniy kutoka Argentina, Vianka Aranky kutoka Honduras na Delfina Dupont kutoka Argentina, wakihudumu kama wajitolea katika LifeStyleTV na LifeStyleSTAY.

Picha: Habari za TED

Wamishonari sita vijana kutoka Amerika ya Kilatini wanapeleka nguvu mpya katika LifeStyleTV nchini Uswidi, wakifanya kazi ya kushiriki imani na maisha yenye afya katika mojawapo ya maeneo magumu zaidi ya kimishonari duniani — Dirisha la Baada ya Ukristo. Eneo hili ambalo, linalojumuisha sehemu kubwa ya Ulaya, Amerika Kaskazini, na Oceania, linakabiliwa na kupungua kwa kasi kwa mahudhurio ya kanisa na kuongezeka kwa usasa.

Tangu alipokuwa na umri wa miaka 17, Miguel Mamani (26) kutoka Bolivia amejitolea kumtumikia Mungu katika misheni. Mwaka huo, uzoefu wenye nguvu wa neema ya Mungu ulithibitisha wito wa maisha yake: kumtumikia Mungu kwa moyo wote popote anapoongozwa.

“Sikuwahi kufikiria nitasomea ughaibuni, hata zaidi kuhudumu kama mmishonari katika bara lingine. Ni ajabu,” anasema Mamani, akishangaa mwongozo wa Mungu.

Mamani ni miongoni mwa wajitolea sita wa Amerika ya Kuilatini wanaohudumu kwa sasa katika LifeStyleTV, huduma inayoungwa mkono na Divisheni ya Trans-Ulaya na kufanya kazi kwa karibu na Hope Channel Norway na Konferensi ya Yunioni ya Norwe. Lengo lao ni kuwafikia watu katika Dirisha la Baada ya Ukristo — mojawapo ya changamoto kubwa za misheni za kanisa, pamoja na Dirisha la 10/40 na Dirisha la Mijini.

Kulingana na Misheni ya Waadventista, “Dirisha la Baada ya Ukristo linajumuisha Ulaya, Marekani, Kanada, Australia, New Zealand na nchi nyingine zinazotoka kwa haraka katika maadili ya Kikristo, inayoonyeshwa na kupungua kwa ukuaji wa kanisa na kuongezeka kwa uasi wa imani, hasa miongoni mwa vijana.”

Tofauti Kubwa

Mamani anasomea masuala ya mawasiliano katika Chuo Kikuu cha Waadventista cha River Plate (UAP) nchini Argentina. Baada ya miaka mitatu ya masomo, anatumia mwaka mmoja nchini Uswidi kabla ya kurudi kumaliza shahada yake.

Maisha nchini Uswidi ni tofauti kabisa na mji wake wenye shughuli nyingi, Santa Cruz de la Sierra, wenye wakazi milioni 2.4. Bolivia ina Waadventista 137,000 wanaoabudu katika makanisa 550 kati ya idadi ya watu milioni 12.3. Kwa kulinganisha, Konferensi ya Yunioni ya Makanisa ya Uswidi ina takriban washiriki 2,900 katika makanisa 35 kwa idadi ya watu milioni 10.5.

Kujenga Mahusiano na Ulaya Isiyo ya Kidini

LifeStyleTV inaendesha hoteli ndogo ya mapumziko na mgahawa wa mimea chini ya chapa LifeStyleSTAY. Biashara hizi husaidia kujenga uhusiano na jamii na kusaidia lengo la huduma kuwa na uwezo wa kujitegemea kifedha.

Mamani ana jukumu muhimu, iwe ni kuwakaribisha wageni, kutunza mazingira, kuosha vyombo, kupiga picha au kuhariri video — yote yakiwa sehemu ya misheni ya kuwafikia raia wa Ulaya wasio wa kidini.

Kuhudumia Mwili na Nafsi

Vianka Aranky (23) kutoka Honduras ni mjitoleaji mwingine wa Amerika ya Kilatini. Baada ya kupata shahada ya kwanza ya lishe kutoka UAP, hakuwa na uhakika kuhusu hatua yake inayofuata.

“Nifanye nini na maisha yangu sasa?” alijiuliza.

Rafiki yake alimhimiza kujitolea kupitia Huduma ya Wajitoleaji Waadventista, ushauri ambao pia ulitolewa na mwalimu. Baada ya kuomba nafasi kadhaa bila mafanikio, alidhani huenda njia hii haikukusudiwa kwake.

Kisha, bila kutarajia, alialikwa kuhudumu kama mtaalamu wa lishe katika LifeStyleTV nchini Uswidi — nafasi kamili. Alifunga mizigo yake na hivi karibuni alikuwa akifanya kazi katika mgahawa wa LifeStyleSTAY, ambao unatoa milo ya mimea pekee.

Msimu wa kiangazi utakapomalizika, Aranky atatumia utaalamu wake kutoa taarifa za lishe kwa ajili ya vyakula vya mgahawa huo, kuchangia mapishi kwa ajili ya vipindi vya upishi, na kuunda maudhui kwa jarida la LifeStyleVIEW.

“Kwa njia nyingi, ninawasaidia watu katika Ulaya isiyo ya kidini kupata lishe bora kwa mwili na roho,” asema.

Kushiriki Imani Kupitia Afya

Aranky anafurahia fursa za kuingiliana na wageni. Kama mwongozo wa matembezi ya asili, anashiriki ushauri wa afya pamoja na kanuni za kibiblia.

“Nilikuwa naona vigumu kuanzisha mazungumzo na watu wageni, lakini sasa najisikia kujiamini kushiriki afya na imani,” anasema.

Aliyelelewa katika kanisa kubwa la Waadventista, sasa anahudumu katika kanisa dogo linalokutana katika hoteli ya LifeStyleSTAY.

“Hii ni tofauti sana na nyumbani, lakini ni kusudi la kile tunachofanya. Sifanyi uinjilisti wa nyumba kwa nyumba — lugha na utamaduni hufanya hivyo kuwa vigumu — lakini najua kazi yangu inaunga mkono misheni. Na watu wapya wanapokuja kanisani, naweza kuwakaribisha na kuzungumza nao.”

Mkurugenzi Mwenye Shukrani

Claus Nybo, mwanzilishi na mkurugenzi wa LifeStyleTV, ana sifa nyingi kwa wajitolea wa Amerika ya Kilatini.

“Wote wana mtazamo chanya, wakiwa na jicho makini la kutambua kile kinachohitaji kufanywa. Tunafurahi sana kwa jinsi wanavyotusaidia kuwafikia watu wa Skandinavia,” asema Nybo.

Uhalisia Mpya wa Misheni

Wamishonari wa Amerika ya Kilatini wanaohudumu barani Ulaya wanaakisi enzi mpya ya misheni ya kimataifa — watendakazi wakihama kutoka kila mahali kwenda kila mahali.

Hii inaakisi wito wa rais wa sasa wa Konferensi Kuu ya Kanisa la Waadventista wa Sabato, Erton Köhler, katika kikao cha 2025 huko St Louis, “Ikiwa tunataka kumwona Yesu akirudi, huu ndio wakati wa kanisa la kimataifa kuinuka kwa nguvu kwa ajili ya misheni.”

Vijana kutoka Amerika ya Kilatini wanaibuka kwa nguvu, wakikabiliana moja kwa moja na changamoto za Dirisha la Baada ya Ukristo.

Makala asili ilichapishwa kwenye tovuti ya habari ya Divisheni ya Trans-Ulaya. Jiunge na Chaneli ya WhatsApp ya ANN kwa habari za hivi punde za Waadventista.

Tor Tjeransen, KOnferensi ya Yunioni ya Norwe

Mada

  • News
  • Youth
  • Dhamira

Makala Husiani

Mada Husiani

Masuala Zaidi