Akiwa anashiriki kwenye gwaride katikati ya jiji la St. Louis siku ya Jumamosi asubuhi, Francis Slay, meya wa jiji hilo, alilishukuru Kanisa la Waadventista wa Sabato kwa kuchagua St. Louis kama mahali pa kufanyia mkutano wake wa kila baada ya miaka mitano.
Akiwa anashiriki kwenye gwaride katikati ya jiji la St. Louis siku ya Jumamosi asubuhi, Francis Slay, meya wa jiji hilo, alilishukuru Kanisa la Waadventista wa Sabato kwa kuchagua St. Louis kama mahali pa kufanyia mkutano wake wa kila baada ya miaka mitano
“Athari ni kubwa sana. Wao [Waadventista] huja St. Louis na kuleta shughuli nyingi katika jiji letu. Wanajaza vyumba vyetu vya mahoteli,” aliambia Adventist World News
“Pia wanafanya jitihada za kidini kupitia St. Louis. Wao ni shirika kubwa, na tunafurahi kuwa nao hapa wiki hii na wiki ijayo,” alisema meya.
Slay hakutoa maelezo maalum kuhusu athari hiyo, lakini alisema anatumaini kuwa na Kanisa la Waadventista tena hivi karibuni jijini.
