Kijana Huko Ekuado Anafundisha Juu ya Mungu Kupitia Sanaa

South American Division

Kijana Huko Ekuado Anafundisha Juu ya Mungu Kupitia Sanaa

Dámaris Paredes anachora michoro ya kiinjilisti na kuwaalika wengine kushiriki katika kikundi chake kidogo huko Ventanas, Ekuado

"Ninatengeneza michoro kwa kadi ili kuwaalika marafiki zangu kwenye shughuli za kanisa, nina hakika kwamba Mungu alinipa zawadi hii ya kipekee, na ninaitumia kwa ajili ya huduma na kazi yake," asema Dámaris Paredes, kijana mwenye umri wa miaka 13 na mshiriki katika Kanisa la Waadventista Wasabato la North Ventanas huko Ventanas, Ecuador.

Wakati wa uzambazaji wa kitabu cha umisionari, Pambano Kuu, Paredes alitayarisha kadi za kibinafsi kwa ajili ya kujitolea na kuwaalika marafiki zake kuhudhuria programu za kanisa lake wakati wa wiki ya Pasaka. Wao, wakichochewa na mwaliko wa Paredes, walikubali, na wakapendezwa kujifunza Biblia kutokana na hilo.

Dámaris, upande wa kushoto, pamoja na rafiki yake wakieneza evanjeli tineja mwingine. [Picha: Mawasiliano ya MES]
Dámaris, upande wa kushoto, pamoja na rafiki yake wakieneza evanjeli tineja mwingine. [Picha: Mawasiliano ya MES]

Paredes anatambua hitaji lililopo la kuhubiri injili, na anatoa sifa maalum kwa wazazi wake kwa usaidizi na msukumo wa kutafuta vijana zaidi ili waweze kumjua Mungu. Pia alionyesha uthamini kwa ajili yao wakiimarisha maisha yake ya kiroho na uhusiano wake pamoja na Mungu.

“Wazazi wangu hunisaidia sana. Wao huandamana nami kwenye ziara, hunifundisha jinsi ya kuzungumza na mtu fulani, na jinsi ya kutoa mafunzo ya Biblia; wanatenga wakati maalum kwangu, na niligundua jinsi ilivyo muhimu kutoa zawadi zangu kwa Kristo, na ndio maana nilianza kuchora jumbe kutoka kwa Yesu na kuzishiriki, hata nikaunda ukurasa, Adventist Online Gallery, kuzichapisha, na marafiki zangu wanapenda sana." anasema.

Kikundi Kidogo cha Vijana kutoka kwa Damaris. [Picha: Mawasiliano ya MES]
Kikundi Kidogo cha Vijana kutoka kwa Damaris. [Picha: Mawasiliano ya MES]

Paredes ni kiongozi wa kikundi chake kidogo cha vijana ambaye anaajiri watu zaidi ili kufungua darasa la Biblia pamoja na mwalimu wake wa vijana. Kwa sasa ana watu sita anaowatembelea na kuwafundisha kuhusu Yesu.

“Nataka kumtumikia Mungu kwa sababu dhabihu aliyoitoa iliniathiri, na ninahitaji watu kujua kwamba wana thamani hiyo na kwamba tayari amelipia gharama kubwa kwa ajili yao. Mungu anawapenda wanadamu na kila mtu anapaswa kujua; Wazazi wangu wameniagiza kumtumikia Kristo, na wanahusika sana na wokovu wangu, na mimi ninahisi vivyo hivyo, na jukumu la kuhubiri upendo wa Mungu kwa watu wengi zaidi,” anasema kijana huyo.

Kama yeye, vijana kadhaa kutoka kusini mwa nchi wamejitolea kwa utume wa Kanisa, kuzungumza, kuhubiri, kushiriki, na kufanya kazi kwa upendo na kutia moyo, kupitia njia ya Kristo, kufanya marafiki na kuwajali wengine.

Sanaa na Damaris. [Picha: Mawasiliano MES]
Sanaa na Damaris. [Picha: Mawasiliano MES]