• Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

The official news channel of the Seventh-day Adventist Church.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Trademark and logo usage
  • Legal notice
  • Privacy policy
© 2026 General Conference Corporation of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike Silver Spring, MD 20904-6601 United States +1-301-680-6000
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
  • Media
  • Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
Seventh Day Adventist Logo

ANN and Adventist.news are the official news channels of the Seventh-day Adventist church.

Seventh-day Adventists are devoted to helping people understand the Bible to find freedom, healing, and hope in Jesus.

Learn more

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

North American Division

Wajitolea Waadventista Waungana kwa Ajili ya Urejesho wa Kimbunga Helene

Wanafunzi na wengine wanahudumu katika baadhi ya jamii zilizoathiriwa zaidi.

October 14, 2024
October 14, 2024
Kikundi cha wajitolea wa 2Serve, waliokuwa wakipokea mafunzo ya kuitikia wakati wa dharura. Baada ya Kimbunga Helene, ilibidi wafupishe mafunzo yao na kuanza kuchukua hatua mara moja.

Kikundi cha wajitolea wa 2Serve, waliokuwa wakipokea mafunzo ya kuitikia wakati wa dharura. Baada ya Kimbunga Helene, ilibidi wafupishe mafunzo yao na kuanza kuchukua hatua mara moja.

[Picha: Huduma na Walei na Viwanda ya Waadventista]

Wakati Kimbunga Helene kilipokuwa kikikaribia kusini-mashariki mwa Marekani, timu kutoka Heritage Academy iliyoko Tennessee tayari ilikuwa ikihusika katika mafunzo ya maandalizi ya majanga katika Shule ya Mount Pisgah Adventist Academy.

Ikiongozwa na 2Serve, huduma ya kukabiliana na majanga na mafunzo inayoongozwa na Jim Ingersoll na kushirikiana na Heritage Academy, timu ya viongozi wanafunzi na wafanyakazi walikuwa wakifundisha wanafunzi jinsi ya kuitikia wakati wa dharura. Lakini kadiri Helene ilivyozidi kupata nguvu na njia yake kuwa isiyotabirika, ilibidi wafupishe mafunzo hayo.

Timu hiyo ilirejea nyumbani haraka, ikinusurika na barabara zilizoharibika, lakini baada ya siku chache walirudi tena North Carolina — safari hii kusaidia jamii iliyozunguka Fletcher Academy huko Fletcher, eneo lililokuwa limekumbwa na uharibifu mkubwa.

“Ilikuwa ni kwa uongozi wa Mungu,” alisema Debbie Baker, rais wa Heritage Academy na rais wa Adventist-Laymen’s Services and Industries (ASi) Tawi la Kusini. “Tulirejea nyumbani muda mfupi kabla ya barabara kuu kuharibiwa, kisha tukajiandaa upya mara moja kusaidia Fletcher Academy na jamii inayozunguka.”

Harakati hii ya haraka iliweka msingi wa ushirikiano mkubwa kati ya huduma za wanachama wa ASi, Heritage Academy, na Fletcher Academy, pamoja na jamii pana ya Waadventista, wakiwemo waumini wa kawaida, wanafunzi wa vyuo vikuu, wawakilishi wa Mkutano wa Carolina wa Kanisa la Waadventista, na wengineo, wakionesha jinsi imani na huduma vinavyoweza kuleta matumaini na uponyaji katikati ya janga.

2Serve imekuwa ikihusika kikamilifu katika kukabiliana na majanga kwa karibu miaka 20, ikifundisha wanafunzi kuhudumu wakati wa dharura kama Kimbunga Katrina.

“Tuliona jinsi vijana walivyobadilika kupitia huduma yao kwa wengine waliokuwa katika wakati wa uhitaji mkubwa. Inawapa nafasi ya kufikiria zaidi ya maslahi yao binafsi na kuona tofauti wanayoweza kuleta,” Baker alieleza. Katika juhudi za kurejesha hali baada ya kimbunga Helene, kazi yao ilizidi kuwa ya kushirikiana zaidi na mashirika ya Waadventista waliporejea kusaidia jamii ya Fletcher.

Fletcher Academy, iliyoko magharibi mwa Carolina Kaskazini, iliepuka uharibifu mkubwa kwenye chuo chake, lakini jamii inayozunguka iliathirika pakubwa. Nyumba zilifurika, barabara zilifungwa, na wakaazi waliachwa bila umeme au maji.

Makamu mkuu wa Fletcher, Brad Durby, alishiriki kwenye mitandao ya kijamii jinsi Kanisa la Waadventista Wasabato la Fletcher lilivyofungua milango yake kwa watu wa kujitolea. "Kuna maelfu ya watu wa kujitolea chini wanaofanya wawezavyo kuleta faraja kwa wale wanaohitaji na wale ambao wamepata hasara kubwa," Durby alisema. "Kanisa letu la Fletcher la Waadventista Wasabato ni 'msingi wa nyumbani' kwa mojawapo ya vikundi vingi, likifanya kile ambacho Yesu alifanya ... akiwaponya wale waliokuwa wakiteseka lakini pia kuwahudumia kwa wakati mmoja."

Jim Ingersoll (kushoto), kiongozi wa kikundi cha kukabiliana na maafa cha 2Serve, wakitoa mafunzo kwa wajitoleaji.
Wanafunzi wawili wa kujitolea wakisaidia kusafisha matope katika moja ya nyumba zilizoathiriwa na Kimbunga Helene.

Durby pia alishiriki kwamba Ingersoll aliwakumbusha wajitolea “kutenga muda wa kusikiliza” watu waliokuwa wakiwasaidia na “kutohusika sana na msaada wa kimwili kiasi cha kukosa fursa ya ‘wakati wa Yesu.’”

Ushirikiano kati ya mashirika hayo ulikuwa muhimu katika kusaidia timu kutoka taasisi zote mbili kushirikiana na wanajamii, washiriki wa kanisa, na wajitolea kutoka maeneo ya karibu na mbali. Waliondoa vifusi, wakaweka vituo vya usambazaji wa mahitaji muhimu (PODs), na pia wakatoa msaada wa kiroho. “Hatutoi msaada wa kimwili pekee,” alisema Baker. “Tunatoa maombi, tunagawa vitabu, na tunachukua muda kuungana na watu walioumizwa.”

Kwenye kila POD, wajitolea waliweka vituo vya maombi, wakialika wanajamii kupokea msaada wa kiroho pamoja na misaada mingine. Mmoja wa vijana wa Heritage Academy, ambaye mwanzoni alikuwa na haya ya kuongoza maombi, alitumia siku nzima kwenye kituo cha maombi, akiombea waathiriwa. “Hizi ni uzoefu unaobadilisha maisha ya vijana,” Baker alisema. “Kuombea mtu na kushuhudia athari yake ni kitu ambacho huwezi kufundisha darasani.”

Kiini cha juhudi hizi za uokoaji kilikuwa si tu kazi iliyokuwa ikifanyika, bali pia imani iliyokuwa ikishirikiwa. Wajitolea waliondoa mali zilizoathiriwa na mafuriko kutoka kwa nyumba za wakazi, zikiwemo samani zilizolowa, kuta za ndani, vifaa vya kuhami joto, na sakafu, katika mchakato uitwao "muck-out." Walisaidia pia kuondoa miti iliyokuwa imeanguka. Baada ya kila kazi ya kusafisha au kuondoa miti, wajitolea walikusanyika na wamiliki wa nyumba kwa ajili ya maombi.

Moja ya desturi zinazopendwa zaidi na Heritage Academy ni kuimba wimbo Still baada ya kumaliza kazi, wakikumbusha wamiliki wa nyumba kwamba hawako peke yao.

“Ni wakati wenye nguvu,” Baker alisema, akitambua unyeti wa kazi hiyo, kwani maisha ya watu yalikuwa yamevurugwa ghafla. “Wanalazimika kutupa vitu vyenye kumbukumbu muhimu. Tunatumaini wanapata faraja kwa kujua kuwa hata tunapoondoka, Mungu yuko pamoja nao.”

Hadithi moja inamhusu Janet, mwanamke wa eneo hilo ambaye alisali kwa msaada asubuhi hiyo kabla ya wajitolea kufika nyumbani kwake. Walipobisha mlangoni na kujitolea kumsaidia, aliwaita “malaika wake.”

“Hakuwa amewasiliana na yeyote, lakini tulikuwa kwenye mtaa huo na tukatokea,” Baker alisimulia. Wajitolea walimsaidia Janet kusafisha nyumba yake na pia wakampa msaada wa kiroho na kihisia.

Juhudi hizi zilipanuka zaidi ya shule hizo mbili. Taasisi kama Wildwood Health Institute na Southern Adventist University zilituma timu zao kusaidia, na watu binafsi kutoka jamii ya Waadventista pia walikuja. “Ushirikiano ni ufunguo,” Baker alisema. “Tuko imara zaidi tunapofanya kazi pamoja.” Takriban asilimia 65 ya wajitolea walikuwa tayari wamepata mafunzo ya Community Emergency Response Team (CERT) kupitia 2Serve na waliweza kuongoza haraka juhudi hizi.

Familia za wenyeji, ingawa zilikumbwa na changamoto za dhoruba, pia zilijitokeza kusaidia. “Ilikuwa ya kushangaza,” Baker alisema. “Watu waliokuwa hawana umeme au maji majumbani kwao walikuja kuwasaidia wengine.”

Kanisa la Waadventista la Fletcher likawa kitovu cha juhudi hizi, likifungua milango yake kwa ajili ya kuwahifadhi wajitolea na kutumika kama kituo cha operesheni. “Tulilala sakafuni, na karibu kila chumba kilitumiwa kwa kitu fulani,” Baker alisema. “Tulikuwa na hadi wajitolea 200 wakiingia na kutoka kwa muda wa wiki nzima.”

Juhudi za urejesho kutoka kwa Kimbunga Helene zikiendelea, na wakati Florida ilijiandaa kukabiliana na hatari za Kimbunga Milton kinachotarajiwa kutua, Baker aliwahimiza watu kuunga mkono huduma hizi kwa njia mbalimbali. “Kama huwezi kujitolea kimwili, fikiria kutoa msaada wa kifedha. Inachukua rasilimali nyingi kuwalisha na kuwahifadhi wajitolea walioko kazini.”

Kwa wale wanaotaka kushiriki moja kwa moja, 2Serve inatoa mafunzo ya CERT, ambayo yanawaandaa watu kuitikia majanga katika jamii zao. “Si swali la iwapo janga litatokea, bali ni lini,” Baker alisema. “Kujiandaa kunakupa nafasi ya kuleta mabadiliko halisi.”

Kupitia ushirikiano wa 2Serve, Heritage Academy, Fletcher Academy, na jamii ya Waadventista, juhudi hizi za urejesho zimeonesha nguvu ya huduma inayotokana na imani. “Sote tuko katika hali ya udhaifu,” Baker alisema, “lakini tunaweza kuleta matumaini na uponyaji kwa wale wanaohitaji zaidi.”

Makala asili ya hadithi hii lilichapishwa kwenye tovuti ya habari ya HUduma ya Walei na Viwanya ya Waadventista (ASi). Heritage Academy na Fletcher Academy ni shule za mabweni zinazojiendesha zenyewe na haziko chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Kanisa la Waadventista.

Topics

  • Humanitarian
  • News
  • Service

Related articles

European Adventist Youth Congress encourages youth to 'choose God’s more'

European Adventist Youth Congress encourages youth to 'choose God’s more'

August 19, 2026

Youth

Bangladesh launches theology education program for lay pastors

Bangladesh launches theology education program for lay pastors

August 18, 2026

Education

In the United States, AdventHealth Heart of Florida and community partners donate thousands of school supplies

In the United States, AdventHealth Heart of Florida and community partners donate thousands of school supplies

August 18, 2026

Education

ADRA assesses damage after magnitude 7.7 earthquake strikes Indonesia

ADRA assesses damage after magnitude 7.7 earthquake strikes Indonesia

August 18, 2026

Humanitarian

Subscribe for our weekly newsletter

Related Topics

More topics

Humanitarian

Free healthcare provided to communities in the Solomon Islands

Free healthcare provided to communities in the Solomon Islands

July 29, 2026
July 12, 2026

Australian government partners with Adventist Aviation

July 5, 2026

In the Solomon Islands, ADRA provides seeds to strengthen food security

May 4, 2026

ADRA Responds to Cyclone Maila, Assisting Victims in the Solomon Islands

More from Humanitarian

Service

Adventists honored by Kiribati government for service

Adventists honored by Kiribati government for service

August 3, 2026
April 22, 2026

Adventist Cyclists in South Australia Raise Funds for Global Aid Initiatives

April 11, 2026

ADRA Prepares Response After Cyclone Maila

April 5, 2026

Mass Clean-up Across Honiara Supports Solomon Islands for Christ Preparations

More from Service

Events

Teamwork makes the dream work at Solomons for Christ

Teamwork makes the dream work at Solomons for Christ

July 19, 2026
July 17, 2026

Bradshaw challenges communicators to keep evangelism at center

July 13, 2026

Adventist communicators build bridges for mission

July 2, 2026

Communicators conference highlights opportunities for digital evangelism

More from Events