• Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

The official news channel of the Seventh-day Adventist Church.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Trademark and logo usage
  • Legal notice
  • Privacy policy
© 2026 General Conference Corporation of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike Silver Spring, MD 20904-6601 United States +1-301-680-6000
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
  • Media
  • Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
Seventh Day Adventist Logo

ANN and Adventist.news are the official news channels of the Seventh-day Adventist church.

Seventh-day Adventists are devoted to helping people understand the Bible to find freedom, healing, and hope in Jesus.

Learn more

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

Ukrainian Union Conference

Kongamano la Vijana Lachochea Misheni na Ufikiaji Nchini Ukraine

Iliofanyika Bucha, kongamano la “Sauti” liliunganisha ibada, ufikiaji, na hisani ili kuwatia moyo vijana kuwa wajumbe wa tumaini na matendo.

June 14, 2025

Ukraine

Valentyn Zahreba, Konferensi ya Yunioni ya Ukraine
Kongamano la Vijana Lachochea Misheni na Ufikiaji Nchini Ukraine

Picha: Konferensi ya Yunioni ya Ukraine

Kuanzia Mei 15 hadi 18, 2025, jiji la Bucha katika mkoa wa Kyiv lilikuwa mwenyeji wa kongamano la vijana Sauti, likiwaleta pamoja zaidi ya washiriki 500 kwa wikendi ya kujifunza, uinjilisti, michezo, na mipango ya hisani.

Kaulimbiu, “Sauti Yako Itasikika,” ililenga kuonyesha maono ya eneo hilo ya kuwawezesha vijana kwa ajili ya huduma hai katika jamii zao na kueneza Injili.

Jumla ya washiriki 410 walijiandikisha rasmi, wakajiunga na wanafunzi kutoka Taasisi ya Sanaa na Sayansi ya Ukraine na Taasisi ya Theolojia ya Waadventista ya Ukraine (UATI), ambapo tukio lilifanyika katika kampasi yao ya pamoja. Jumamosi (Sabato), pamoja na wageni waliotembelea, mahudhurio yalizidi 600.

Ibada za asubuhi na jioni zilijumuisha ujumbe kutoka kwa wachungaji Volodymyr Velechuk, Nazar Yarovyi, Volodymyr Borovyi, Leonid Rutkovskyi, na Ivan Romaniuk. Wakati wa mchana, washiriki walihudhuria vikao na shughuli zilizoundwa kuwapa maarifa ya kiroho na zana za kiutendaji kwa ajili ya utume.

Kila asubuhi ilianza na matembezi ya maombi saa 6 asubuhi ikifuatiwa na ibada, na kila jioni ilihitimishwa na majadiliano ya vikundi vidogo vilivyojikita kwenye mada ya siku.

Ivan Romaniuk, kiongozi wa Huduma za Vijana Waadventista nchini Ukraine, alisisitiza dhamira ya kipekee ya tukio hilo.

“Kongamano letu la vijana lililopita, ‘Nuru Katika Giza’, lilifanyika chini ya mwaka mmoja uliopita, Juni 2024. Sauti ina ujumbe, utume, na huduma ya umma iliyo na lengo zaidi. Kichwa hicho kinarejelea Yohana Mbatizaji, ambaye alisema yeye ni sauti tu — si shujaa, bali mjumbe. Tunaamini vijana wa leo wameitwa kuwa sauti hiyo, wakitangaza ujumbe wa Mungu kabla ya kurudi kwa Kristo,” alisema Romaniuk.

Romaniuk alieleza zaidi jinsi mada ya kongamano ilivyoundwa.

“Tuliwaomba wazungumzaji kuchunguza wazo la utume kwa kutumia sitiari ya mavuno — maandalizi, kupanda, kulea, kuvuna, na kuhifadhi. Warsha zilifuata mzunguko huu wa kimisheni.”

Jioni ya Sabato, uinjilisti wa mijini ulifanyika Bucha, Irpin, na Hostomel, ambapo vijana 125 katika timu 25 waliweka maeneo ya ufikiaji wa umma. Licha ya hali ya hewa baridi na mvua, wengi waliripoti mazungumzo yenye maana na athari ya kiroho.

“Baadhi ya shughuli za mitaani zilikatizwa na hali ya hewa, lakini matokeo halisi yalikuwa ni uzoefu wa kuunganishwa,” alishiriki Vlad Mikula, mratibu wa mpango huo. “Kijana mmoja tuliyezungumza naye wakati wa mchana hata alikuja kwenye kongamano jioni hiyo.”

Sabato ilihitimishwa na sherehe ya ubatizo, ambapo vijana watano walitoa maisha yao kwa Kristo. Velechuk aliwahutubia waliobatizwa wapya.

“Libebe jina la Bwana kwa heshima. Njia iliyo mbele si rahisi, lakini ni ya heshima. Endelea kukua ndani Yake.”

Jumapili, Mei 18, mbio za hisani zilizoandaliwa kwa ushirikiano na klabu ya mazoezi ya Clan zilikusanya washiriki 29 wa vijana. Lengo: kukusanya fedha kwa ajili ya Hospitallers kikosi cha matibabu cha kujitolea, ambacho kituo chake huko Pavlohrad kiliharibiwa katika shambulio la kombora Aprili 25, 2025.

Sehemu ya chakula katika kongamano ilitoa mapato yake ya siku hiyo kwa ajili ya kusaidia jambo hilo. Jumla ya hryvnia 30,000 (takriban dola 700 za Kimarekani) zilichangishwa. Washindi wa juu katika makundi ya wanaume na wanawake walitunukiwa zawadi. Michango bado inakaribishwa kupitia jukwaa la misaada la Monobank.

Tukio lilipohitimishwa, Romaniuk alitafakari juu ya maana yake ya kina.

“Katika kila tunalofanya, kinachojalisha zaidi si muundo au tukio lenyewe — ni watu. Vijana wanaohitaji wokovu.”

Matukio ya vijana kama Sauti hufanyika ndani ya kanisa na katika ulimwengu mpana kwa ajili yao na kuwasaidia kuanza safari yao kuelekea kumjua Mungu.

Makala alisi ilitolewa na Konferensi ya Yunioni ya Ukraine. Jiunge na Chaneli ya WhatsApp ya ANN kwa habari za hivi punde za Waadventista.

Valentyn Zahreba, Konferensi ya Yunioni ya Ukraine

Topics

  • News

Related articles

Nova Esperança School's values encourage non-Adventist families to send children

Nova Esperança School's values encourage non-Adventist families to send children

August 9, 2026

Education

Adventist Church workers deploy across northern Botswana for week of ministry

Adventist Church workers deploy across northern Botswana for week of ministry

August 8, 2026

Ministries

GAiN offers to support digital ministry in New Zealand

GAiN offers to support digital ministry in New Zealand

August 8, 2026

Media

Ellen White’s 'Welfare Ministry' to be reissued as 'Christian Service, Volume 2'

Ellen White’s 'Welfare Ministry' to be reissued as 'Christian Service, Volume 2'

August 7, 2026

Press Release

Subscribe for our weekly newsletter

Related Topics

More topics

Children

Two Churches Open to Support Neurodiverse Children and their Families

Two Churches Open to Support Neurodiverse Children and their Families

May 13, 2026
March 27, 2026

Children Lead Worship and Outreach During Global Children’s Day in Papua New Guinea

More from Children

Ministries

Sydney women share practical skills and hope in the Solomon Islands

Sydney women share practical skills and hope in the Solomon Islands

August 2, 2026
August 2, 2026

Health team in the Solomon Islands delivers care behind prison walls

July 30, 2026

French Polynesia invests in young digital disciples

July 29, 2026

Free healthcare provided to communities in the Solomon Islands

More from Ministries