• Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

The official news channel of the Seventh-day Adventist Church.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Trademark and logo usage
  • Legal notice
  • Privacy policy
© 2026 General Conference Corporation of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike Silver Spring, MD 20904-6601 United States +1-301-680-6000
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
  • Media
  • Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
Seventh Day Adventist Logo

ANN and Adventist.news are the official news channels of the Seventh-day Adventist church.

Seventh-day Adventists are devoted to helping people understand the Bible to find freedom, healing, and hope in Jesus.

Learn more

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

Inter-American Division

Divisheni ya Baina ya Amerika Kuwakusanya Wachungaji Wake Katika Matukio Matatu ya Kihistoria ya Kihuduma

Karibu wachungaji 4,000 watashiriki katika mapumziko ya kichungaji mnamo Septemba 2024.

September 2, 2024
September 2, 2024
Divisheni ya Baina ya Amerika Kuwakusanya Wachungaji Wake Katika Matukio Matatu ya Kihistoria ya Kihuduma

[Picha: Divisheni ya Baina ya Amerika]

Kwa wiki tatu za kwanza za Septemba, Divisheni ya Baina ya Amerika (IAD) itajaribu kitu ambacho hakijawahi kuwezekana kwa zaidi ya miaka 100 tangu ilipopangwa: Kukusanya zaidi ya wachungaji wake Waadventista Wasabato 3,000 kwa siku nne ya mapumziko.

Takriban wahudumu 4,000, wengi wao wakiwa wachungaji wa makanisa ya mtaa, wanaochunga zaidi ya makutaniko 23,000 katika eneo la IAD, watashiriki katika mafungo matatu ya huduma ambayo yatafanyika Mexico, Jamhuri ya Dominika na El Salvador. Wachungaji kutoka Cuba, Venezuela na Haiti wataweza kuunganishwa kwa mbali ili kushiriki katika shughuli za mafungo katika nchi zao.

Ni wazo ambalo limekuwa likitengenezwa kwa miaka mingi, waandaaji walisema. Mafungo ya kwanza yataanzia Cancun, Mexico, kukiwa na karibu wachungaji 2,000 na wenzi wao kutoka Mexico, Kolombia, na Belize, pamoja na Aruba, Bonaire na Curacao, Septemba 2-5, 2024. Takriban wachungaji 1,000 na wenzi wao kutoka Kanisa la Visiwa vya Karibea vinavyozungumza Kiingereza na Kihispania na, pamoja na Martinique, Guadelope na Guiana ya Ufaransa vitakusanyika Punta Cana, Jamhuri ya Dominika, mnamo Septemba 9-12. Zaidi ya wachungaji 700 na wenzi wao kutoka nchi za Amerika ya Kati watakutana El Salvador, Septemba 16-19.

"Tumefanya mikutano ya eneo nzima, mafunzo na matamasha kwa walei, kambi za vijana, mikutano ya wainjilisti wa viabu, matukio ya uhuru wa kidini na mengine mengi, lakini wale wanaoongoza makanisa na makutaniko hawajawahi kupata nafasi ya kujitenga na makongamano yao kwa ajili ya mafungo pamoja katika kiwango hiki cha [divisheni]," alisema Josney Rodríguez, katibu wa Chama cha Wahudumu wa IAD.

Wachungaji katika IAD kawaida huongoza makutaniko manne, matano, au zaidi katika wilaya zao. Baadhi ya wachungaji hadi makutaniko 30. Kuchukua siku chache mbali na ratiba zao kamili kutaburudisha kwa njia nyingi, alielezea Rodríguez. Hilo litawezekana kutokana na maelfu ya wazee wa kanisa wanaosaidia katika kuchunga kundi katika yunioni 24 za IAD, aliongeza.

"Kuna msisimko mwingi kuwakusanya na kuwaheshimu wengi sana ambao wako mstari wa mbele kusimamia makutaniko yetu yanayokua," Rodríguez alisema. Nchini Cuba, kwa mfano, kanisa litakusanya wachungaji 350 na wenzi wao ili kuungana kwa mbali wakati wa mafungo ya pili katika eneo zima, alisema Rodriguez. Vile vile, wachungaji kutoka Yunioni za Mashariki na Magharibi ya Venezuela pia watakusanya wachungaji wao na kuunganishwa kwa mbali wakati wa tukio la mafungo la Jamhuri ya Dominika.

"Wachungaji ndio safu ya kwanza ya ulinzi huko nje katika maelfu ya Makanisa yetu ya Waadventista Wasabato, na ni muhimu kurudi nyuma na kupata upako wa kiroho katikati ya changamoto na majukumu mengi wanayokabiliana nayo," alielezea Rodríguez.

Chini ya mada 'Waliotiwa Mafuta,' mafungo haya yataangazia haja ya Roho Mtakatifu kuongoza na kufanya kazi katika maisha ya wachungaji na familia zao wanapofanya kazi pamoja kuhudumia makongamano na jamii zao katika maandalizi ya Kurudi kwa Pili kwa Yesu," alisema Rodríguez. "Tunataka kuona wachungaji wetu wakihuisha upya ahadi yao kwa mwito wao wa kichungaji, familia zao, na kuwa na uhusiano wa kina na Mungu wanapoendelea kutekeleza utume," alisema.

Wachungaji na wenzi wao watasali pamoja, watashiriki katika semina, mawasilisho, na shughuli za burudani, watapata fursa ya ushauri wa kibinafsi wa familia, na kufahamiana na wenzao kutoka kote nchini na visiwa katika IAD.

“Mafungo haya yatawawezesha wachungaji na wenzi wao kutumia muda wa pekee pamoja, kuangalia majukumu yao kama viongozi, kama familia, kutafuta uwiano katika maisha yao, na kupata nguvu wanapohudumu katika huduma,” alisema Rodríguez. “Sio rahisi kushughulika na changamoto za watu, hisia, masuala katika kutaniko, kusimamia ujenzi wa kanisa, kuongoza ukuaji wa washiriki, kuongoza mikutano ya bodi, na mengine mengi zaidi,” aliongeza. “Wachungaji si watu wenye uwezo zaidi wa kibinadamu; wanahitaji muda wa kupumzika, kuhisi wamechangiwa tena, na kuhudumiwa ili kuendelea kuwatayarisha wengine kwa ajili ya Ufalme.”

Wasemaji kutoka Konferensi Kuu ya Kanisa, Divisheni ya Baina ya Amerika, na Divisheni ya Amerika Kusini watashiriki wakati wa hafla za mafungo ya siku nne.

Makala asili ilichapishwa kwenye tovuti ya Divisheni ya Baina ya Amerika

Topics

  • News

Related articles

Adventist Church in Mexico unveils mobile production truck

Adventist Church in Mexico unveils mobile production truck

August 21, 2026

Media

East-Central Africa Division content creators challenged to turn influence into mission

East-Central Africa Division content creators challenged to turn influence into mission

August 20, 2026

Media

Atlantic Union Conference dedicates new headquarters during grand opening

Atlantic Union Conference dedicates new headquarters during grand opening

August 20, 2026

Events

Inter-America’s digital creators mobilize for OneVoice27

Inter-America’s digital creators mobilize for OneVoice27

August 19, 2026

OneVoice27

Subscribe for our weekly newsletter

Related Topics

More topics

Events

Teamwork makes the dream work at Solomons for Christ

Teamwork makes the dream work at Solomons for Christ

July 19, 2026
July 17, 2026

Bradshaw challenges communicators to keep evangelism at center

July 13, 2026

Adventist communicators build bridges for mission

July 2, 2026

Communicators conference highlights opportunities for digital evangelism

More from Events

Nature

In the Solomon Islands, ADRA provides seeds to strengthen food security

In the Solomon Islands, ADRA provides seeds to strengthen food security

July 5, 2026
More from Nature

Service

Adventists honored by Kiribati government for service

Adventists honored by Kiribati government for service

August 3, 2026
May 4, 2026

ADRA Responds to Cyclone Maila, Assisting Victims in the Solomon Islands

April 22, 2026

Adventist Cyclists in South Australia Raise Funds for Global Aid Initiatives

April 11, 2026

ADRA Prepares Response After Cyclone Maila

More from Service