• Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

The official news channel of the Seventh-day Adventist Church.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Trademark and logo usage
  • Legal notice
  • Privacy policy
© 2026 General Conference Corporation of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike Silver Spring, MD 20904-6601 United States +1-301-680-6000
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
  • Media
  • Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
Seventh Day Adventist Logo

ANN and Adventist.news are the official news channels of the Seventh-day Adventist church.

Seventh-day Adventists are devoted to helping people understand the Bible to find freedom, healing, and hope in Jesus.

Learn more

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

Inter-European Division

Balozi wa Kenya Azuru Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede ili Kuimarisha Ushirikiano wa Kimatibabu

Hospitali iliyoko Berlin inaongeza juhudi za kusaidia waathirika wa ukeketaji wa wanawake kupitia ushirikiano na wataalamu wa afya wa Kenya.

February 25, 2025

Ujerumani

Martin Knoll, Habari za Divisheni ya Baina ya Ulaya
Balozi wa Kenya Azuru Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede ili Kuimarisha Ushirikiano wa Kimatibabu

Picha: Krankenhaus Waldfriede / Martin Knoll

Ukeketaji wa sehemu za siri za wanawake (FGM) ni hali ya kusikitisha hata katika nchi ya Kiafrika ya Kenya. Ingawa marufuku ya FGM imewekwa kisheria nchini Kenya tangu 2011, desturi hii bado imeenea katika baadhi ya maeneo. Wasichana na wanawake ni waathirika wa desturi hii, ambayo ina madhara makubwa ya kimwili na kisaikolojia.

Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede huko Zehlendorf, Berlin, inatibu wanawake na wasichana walioathirika. Kituo cha Desert Flower, ambacho kiko katika hospitali hiyo, kilianzishwa kwa madhumuni haya tarehe Septemba 11, 2013. Wanawake walioathirika wanapewa upasuaji hapa, wanarejeshwa kimwili kwa njia bora zaidi, na pia wanapata msaada wa kisaikolojia.

Timu ya madaktari inayojumuisha Madaktari Wakuu Dkt. von Frischen, Dkt. Scherer, na Dkt. Müller, pamoja na Daktari Mwandamizi Dkt. Strunz, imekuwa Kenya mara kadhaa katika miaka ya hivi karibuni kufanya upasuaji kwa wanawake walioathirika katika Kliniki ya Gynocare Fistula huko Eldoret. Pia wamefundisha na kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa ndani katika kliniki hicho nchini Kenya kuhusu matibabu na upasuaji. Wafanyakazi wa matibabu kutoka Kenya pia wanapewa mafunzo ipasavyo katika Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede.

Mnamo Januari 29, 2025, balozi wa Kenya, Stella Mokaya Orina, alitembelea Hospitali hiyo ya Waadventista ya Waldfriede. Alivutiwa sana wakati wa ziara yake ya idara mbalimbali za hospitali hiyo na Mkurugenzi Mtendaji Bernd Quoß.

Quoß alimkaribisha katika mkutano wa Chama cha Msaada cha Waldfriede r.a (chama kilichosajiliwa). Waldfriede r.a. inafadhili karibu asilimia 100 ya Kituo hicho cha Desert Flower. Orina alishukuru Hospitali ya Waadventista Waldfriede kwa msaada wake. Alisisitiza sana kupanua ushirikiano kati ya Waldfriede na nchi yake, Kenya, na anakusudia kufanya zaidi kufanikisha lengo hilo.

Quoß alishiriki, “Daima imekuwa na itaendelea kuwa jambo la muhimu kwetu kusaidia watu wenye uhitaji mkubwa na kuwezesha matarajio bora na ubora mpya wa maisha kupitia matibabu kama haya - kulingana na taswira yetu kama Kanisa la Waadventista wa Sabato.”

Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede

Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede isiyo ya kifaida huko Berlin ni hospitali ya kufundisha ya Chuo Kikuu cha Charité - Universitätsmedizin Berlin. Charité – Universitätsmedizin Berlin ndiyo hospitali kubwa zaidi ya chuo kikuu barani Ulaya.

Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede imethibitishwa mara kadhaa kulingana na vigezo vya ubora wa kisheria na tayari imepokea tuzo nyingi kwa ubora wake wa matibabu na uuguzi.

Mnamo 2025, Hospitali ya Waldfriede ilitajwa kuwa moja ya hospitali bora zaidi duniani na imethibitishwa ipasavyo.

Hospitali ya Waadventista ya Waldfriede inatibu takriban wagonjwa wa ndani 15,000 na wagonjwa wa nje 120,000 kila mwaka. Inaendeshwa na Kanisa la Waadventista wa Sabato, ambalo lina vituo vya matibabu takriban 450 duniani kote. Waldfriede ni mshirika wa ushirikiano wa Chama cha Hospitali za Waadventista Advent Health nchini Marekani.

Hospitali hii ni sehemu ya mtandao wa afya wa Waldfriede, ambao pia unajumuisha kliniki ya siku, kituo cha huduma za kijamii, chuo cha afya na uuguzi, kampuni ya huduma, kituo cha afya cha “PrimaVita”, kliniki ya kibinafsi ya Nikolassee, na “Kituo cha Desert Flower."

Mtandao wa Waldfriede ni mtoa huduma za matibabu na uuguzi wenye utofauti mkubwa zaidi kusini magharibi mwa Berlin. Ukiwa na wafanyakazi wapatao 950, ni moja ya waajiri wakubwa katika wilaya ya Steglitz-Zehlendorf.

Makala asili ilichapishwa kwenye tovuti ya habari ya Divisheni ya Baina ya Ulaya.

Martin Knoll, Habari za Divisheni ya Baina ya Ulaya

Topics

  • Healthcare
  • News

Related articles

Rural community in Brazil establishes its first Adventist church

Rural community in Brazil establishes its first Adventist church

August 11, 2026

Mission

Adventist Church responds following earthquake in Japan

Adventist Church responds following earthquake in Japan

August 11, 2026

Crisis

Adventist Church reaches Chinese communities in Tonga and Solomon Islands

Adventist Church reaches Chinese communities in Tonga and Solomon Islands

August 11, 2026

Adventist Mission

Adventist Church assesses damage after earthquake strikes Colombia

Adventist Church assesses damage after earthquake strikes Colombia

August 11, 2026

Crisis

Subscribe for our weekly newsletter

Related Topics

More topics

Healthcare

Health team in the Solomon Islands delivers care behind prison walls

Health team in the Solomon Islands delivers care behind prison walls

August 2, 2026
July 29, 2026

Free healthcare provided to communities in the Solomon Islands

July 16, 2026

Adventist health event offers hope for type 2 diabetes

July 12, 2026

Australian government partners with Adventist Aviation

More from Healthcare

Health

Samoan Cookbook Wins International Award for Health-Focused Outreach

Samoan Cookbook Wins International Award for Health-Focused Outreach

April 10, 2026
February 28, 2026

First 10,000 Toes Wellness Centre Opens in Fiji

More from Health

Media

Chinese-language broadcasts expand Adventist outreach in Solomon Islands

Chinese-language broadcasts expand Adventist outreach in Solomon Islands

August 10, 2026
August 8, 2026

GAiN offers to support digital ministry in New Zealand

July 30, 2026

French Polynesia invests in young digital disciples

July 17, 2026

Bradshaw challenges communicators to keep evangelism at center

More from Media