Eneo la Kaskazini mwa Asia na Pasifiki Latoa Mafunzo ya Mtaala Mpya wa Shule ya Sabato

Picha: Divisheni ya Kaskazinimwa Asia na Pasifiki

Northern Asia-Pacific Division

Eneo la Kaskazini mwa Asia na Pasifiki Latoa Mafunzo ya Mtaala Mpya wa Shule ya Sabato

Alive in Jesus inalenga kuwawezesha na kuwatia nguvu wazazi, walezi, walimu wa shule ya Sabato, viongozi, na wengine kuwa mfano na kuendeleza uhusiano unaostawi na Yesu na watoto katika maeneo yao ya ushawishi.

Mnamo Machi 27-28, 2024, tukio muhimu lilifanyika wakati Divisheni ya Kaskazini mwa Asia na Pasifiki (NSD), kwa ushirikiano na Konferensi ya Yunioni ya Korea (KUC) na Mchungaji Kim YoungUn, mkurugenzi wa huduma za watoto wa KUC, walipokutana kutoa mafunzo na kukagua mtaala wa shule ya Saato wa Alive in Jesus. Muktadha huu, uliotengenezwa na Konferensi Kuu, ni chombo muhimu katika kuendeleza ukuaji wa kiroho wa watoto. Wakurugenzi wa huduma za watoto kutoka eneo la NSD na walimu na watafsiri wa KUC walitumia siku mbili kupokea mafunzo na maelekezo kutoka kwa Nina Atcheson, meneja na mhariri mkuu wa mtaala huo mpya wa Alive in Jesus. Vikao vya mafunzo vilivyokamilika vilijumuisha mada mbalimbali, ikiwa ni pamoja na masomo ya juu katika kufundisha elimu ya dini, maendeleo ya tabia kwa watoto, mbinu za kufundisha na kujifunza kwa makundi mbalimbali ya umri, kufundisha watoto wenye mahitaji maalum, sanaa ya kusimulia hadithi, maonyesho ya mbinu za kufundisha, vikao vya mwingiliano wa kikundi, na nyakati za maombi.

“Lengo letu ni kutoa mpito laini kutoka Grace Link kwenda Alive in Jesus, tukiwapa walimu na wazazi zana muhimu za kufanya mtaala huu mpya wa shule ya Sabato kuwa baraka kwa wazazi na watoto wao wanaposoma Biblia pamoja nyumbani. Ni muhimu kushirikiana kwa makusudi na watoto na wazazi wao katika njia hii mpya ya kufundisha na kujifunza,” alisema Raquel Arrais, mkurugenzi wa huduma za watoto wa NSD na muandaaji mkuu wa tukio la mafunzo.

Nina Atcheson alizungumza na viongozi waliohudhuria mkutano huo huko Seoul, Korea, kuhusu falsafa na nguzo za mtaala na jukumu la walimu wa shule ya Sabato. “Tumepewa wito mkubwa si tu kuwakuza watoto wadogo bali pia kuwapa uwezo walimu na wazazi wengi katika Divisheni Kaskazini mwa Asia na Pasiiki,” alisema Atcheson. “Wito huo unajumuisha kufundisha watoto wenye mahitaji mbalimbali kuhusu mambo ya sasa yanayoathiri nyumbani, ikiwa ni pamoja na wasiwasi, msongo wa mawazo, talaka, athari za muda wa kutumia skrini, utata wa jinsia, upungufu wa uhusiano na asili, na zaidi. Nguzo za mtaala zinajumuisha neema inayotolewa na Yesu, maendeleo ya tabia, na misheni. Alive in Jesus inalenga kuwapa uwezo na kuwapa nguvu wazazi, walezi, walimu wa shule ya Sabato, viongozi, na wengine kuwa mfano na kukuza uhusiano unaostawi na Yesu na watoto katika maeneo yao ya ushawishi.”

Nina Atcheson anazungumzia falsafa na nguzo za mtaala pamoja na jukumu la walimu wa shule ya Sabato.
Nina Atcheson anazungumzia falsafa na nguzo za mtaala pamoja na jukumu la walimu wa shule ya Sabato.

Konferensi Kuu inapanga kuzindua mtaala wa Alive in Jesus kuanzia ngazi za Baby na Beginner mwaka wa 2025, Kindergarten na Primary mwaka wa 2026, Junior na Teen mwaka wa 2027, na Youth mwaka wa 2028. Tafsiri ya ngazi ya Baby Steps na Beginner kwenda lugha mbalimbali unaendelea katika eneo la NSD.

Mchungaji Kim Kwon, mkurugenzi wa shule ya sabato ya NSD, alisema, “Alive in Jesus itawezesha watoto kusoma kwa njia inayoendana na mbinu za kisasa za elimu shuleni, hivyo kuwafanya waweze kuyakumbatia mafundisho ya kiroho kama yao wenyewe. Imeundwa kiasi kwamba hata watoto wachanga wanaweza kushiriki masomo ya kiroho na wazazi wao, hii inahitaji ushiriki wa wazazi na kuendeleza ukuaji wao wa kiroho. Hii inatayarisha familia vyema kwa kusubiri Ujio wa Pili.”

Washiriki wanapiga picha za pamoja mwishoni mwa mkutano.
Washiriki wanapiga picha za pamoja mwishoni mwa mkutano.

Makala ya awali yalichapishwa kwenye tovuti ya Divisheni ya Kaskazini mwa Asia na Pasifiki.