• Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
    • ANN Video
    • ANN In-Depth
    • ANN Profiles

The official news channel of the Seventh-day Adventist Church.

  • Facebook
  • Instagram
  • X
  • YouTube
  • Trademark and logo usage
  • Legal notice
  • Privacy policy
© 2026 General Conference Corporation of Seventh-day Adventists
12501 Old Columbia Pike Silver Spring, MD 20904-6601 United States +1-301-680-6000
  • World
  • Americas
  • Asia
  • Europe
  • Middle East & Africa
  • Oceania
  • Media
  • Languages
    • English
    • Français
    • हिन्दी
    • Português
    • Español
    • Kiswahili
  • About ANN
    • Reproduction Requirements
    • Styleguide
  • Subscribe
Seventh Day Adventist Logo

ANN and Adventist.news are the official news channels of the Seventh-day Adventist church.

Seventh-day Adventists are devoted to helping people understand the Bible to find freedom, healing, and hope in Jesus.

Learn more

  • Adventist.org
  • Adventist Mission
  • ADRA
  • Adventist World Radio
  • Hope Channel

West-Central Africa Division

Chuo cha Waadventista cha Sayansi ya Uuguzi Jengre Chafanya Sherehe ya Uzinduzi kwa Wanafunzi 81

Tamaduni ya kuweka kofia na kuweka koti katika taaluma ya uuguzi inaashiria mabadiliko kutoka kwa mafunzo ya kinadharia hadi utunzaji wa wagonjwa kwa vitendo.

October 22, 2024
October 22, 2024
Ezinwa Alozie, Konferensi ya Yunioni ya Kaskazini mwa Nigeria
Sehemu ya wanafunzi wakiwa wanavalishwa Kofia na Makoti ya Uuguzi

Sehemu ya wanafunzi wakiwa wanavalishwa Kofia na Makoti ya Uuguzi

[Picha: Konferensi ya Yunioni ya Kaskazini mwa Nigeria]

Katika tukio la kihistoria, Chuo cha Waadventista cha Sayansi ya Uuguzi cha Jengre (Adventist College of Nursing Sciences Jengre, ACONS -J) kilisherehekea uzinduzi na uvaaji koti kwa wanafunzi wake 81 wa Uuguzi wa Msingi mnamo Ijumaa, Septemba 20, 2024, kuashiria mabadiliko yao kutoka kwa uanafunzi hadi kwa taaluma katika fani ya uuguzi. .

Sherehe hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato la Hospitali ya Jengre, Jengre, Jimbo la Plateau, Nigeria, ilionyesha umuhimu wa kuunganisha imani na masomo kama zana muhimu za utunzaji.

Sherehe ya kuweka kofia na kuvaa koti ni utamaduni uliotukuka katika taaluma ya uuguzi, ikiashiria mabadiliko kutoka kwa mafunzo ya kinadharia hadi kwa vitendo, utunzaji wa wagonjwa, alisema mzungumzaji mgeni, Dk Aridi Elkana Simon, Naibu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi, katika Bodi ya Usimamizi wa Hospitali ya Jimbo la Plateau.

Sehemu ya Wanafunzi Baada ya Sherehe ya Kuvalishwa Kofia na Makoti

Sherehe hiyo, kulingana na yeye: "inaashiria ibada muhimu ya kupita kwa wanafunzi wa uuguzi, ikiashiria kuingia kwao rasmi katika mazoezi ya kliniki na kujitolea kwao kudumisha maadili ya msingi ya uuguzi -- huruma, maadili, na taaluma."

Kofia hiyo, alisema: "Inawakilisha huduma na kujitolea, wakati koti linasimama kama ishara ya uwajibikaji na utayari wa kukumbatia changamoto za taaluma ya uuguzi."

Akizungumzia mada "Imani na Kujifunza: Vyombo Madhubuti vya Kutunza", Dk Simon alibainisha kuwa mchanganyiko wa imani na kujifunza huwawezesha wauguzi kutoa huduma kamili, kushughulikia mahitaji ya kimwili ya wagonjwa na ustawi wao wa kihisia na kiroho.

"Uuguzi sio tu kuhusu utaalamu wa kiufundi; ni kuhusu kutunza mtu mzima - mwili, akili, na roho. Imani na maadili ni muhimu katika kutoa huduma hiyo," alisema.

Kaimu Mwenyekiti, Chuo cha Uzamili cha Uuguzi na Ukunga cha Afrika Magharibi, Tawi la Jimbo la Plateau, aliwahimiza wanafunzi wakumbatie kujifunza kwa afya kwani kungeboresha kuridhika kwa wagonjwa, kuongeza ari, kuchochea matokeo bora ya afya na kuongeza ufanisi na kupunguza makosa.

Hapo awali, Dk. Istifanus Ishaya, rais wa Konferensi ya Yunioni ya Naigeria Kaskazini wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, alitoa changamoto kwa wanafunzi kutopuuza maadili ya huruma, uelewa, ubora, uadilifu, na ustahimilivu katika utunzaji.

"Leo inaashiria hatua muhimu katika safari yenu kama wataalamu wa afya wa siku zijazo. Unapopokea kofia na koti zenu leo hii, sio tu ishara ya mafanikio yako ya kitaaluma lakini ukumbusho wa jukumu kubwa ambalo liko mbele yako."

Aliongeza, “Kubali wito wako, ukijua kuwa uuguzi ni zaidi ya taaluma. Umekabidhiwa utunzaji wa wengine wakati wa hatari zaidi. Kubali fursa hii kwa huruma, kujitolea, na uadilifu."

"Ninapowapongeza leo, nakuhimiza pia kujitolea kujifunza maishani, kulima uvumilivu na usisite kushiriki uzoefu wenu na wenzenu; kwa pamoja mnaweza kuunda mazingira ya kusaidiana. Ninyi ni mustakabali wa huduma ya afya nchini Nigeria na zaidi. Safari yenu kama wauguzi na iwe na alama ya ubora na huruma," Dk. Ishaya aliwahimiza.

Jonathan Precious, mwanafunzi ambaye alitunukiwa kama mwanafunzi bora wa uuguzi, alielezea sherehe hiyo kama "ushahidi wa kutokata tamaa". "Imekuwa safari ya ajabu. Kwa tuzo niliyopewa, najisikia kuwa na changamoto ya kudumisha kasi," alisema kwa shukrani.

Kwa Bali Divine Peter, ambaye alielezea shukrani zake kwa Mungu kwa msaada wa kiroho na kitaaluma ambao amepokea kutoka kwa taasisi hiyo, alifichua kwamba ndoto yake ni kuwa muuguzi maarufu popote atakapokuwa.

Godswill Chichetam, mwanafunzi, alisema: "Sherehe ya kuvalishwa kofia na makoti ni moja ya nyakati bora zaidi niliyopata katika ACONS-J na natumaini kupata nyakati nyingi zaidi katika siku zijazo".

Mwanafunzi mwingine, Irene Agu, alisema imekuwa uzoefu wa ajabu kutoka Jimbo la Lagos hadi kaskazini mwa Nigeria kusoma.

"Nimekuja kuishi ACONS-J, sitaacha shule na hii itakuwa kituo changu cha mwisho na nitawafurahisha wazazi wangu na wale wanaonitegemea. Zaidi ya yote, nitafanikiwa kupitia Kristo anitiaye nguvu," aliomba.

Sehemu ya Wazazi na Washiriki wa Kanisa wakati wa Sherehe hiyo.

Musa Yusuf Madaki ni mwakilishi wa kozi wa wanafunzi waanzilishi wa Uuguzi wa Msingi wa ACONS-J. Kwa mujibu wake, imekuwa safari ya kipekee.

Anasema, “Mungu amekuwa mwaminifu. Ni heshima kubwa kuwa sehemu ya kundi la kwanza la ACONS-J. Sherehe hii ni uzoefu mzuri unaoashiria mwanzo wa jukumu kubwa. Sasa tunachukua jukumu linalohitaji si tu utaalam wa matibabu bali pia huruma, uvumilivu, na uelewa. Naomba Mungu aendelee kutujenga kuwa kitu kikubwa ambacho kitasaidia taifa kwa ujumla.”

Tukio hilo lilikuwa na ujumbe wa busara za heri kutoka kwa baadhi ya wageni mashuhuri, wakithamini uongozi wa chuo kwa kudumisha viwango kama inavyoonyeshwa na utendaji wa jumla wa wanafunzi. Pia waliwapongeza wanafunzi kwa uvumilivu wao, wakiwahimiza kuendelea kujitolea na kuwa na ujasiri katika safari zao za kitaaluma.

Ujumbe mmoja ulitoka kwa Rais aliyepita wa NNUC Yohanna Harry.

Harry aliwasihi wanafunzi waamini mfumo na kujitahidi kuwa bora zaidi. Alisema, “Hatuwezi kushindana na mtu yeyote. Zingatia masomo yako na kuwa kile unachotaka kuwa. Kuhusu taaluma ya uuguzi, anga ni mwanzo wa mafanikio yako.”

Tukio hilo liliudhuriwa na viongozi wa kanisa na washiriki wataalamu wa uuguzi kutoka Bodi ya Usimamizi wa Hospitali ya Jimbo la Plateau na Hospitali ya Waadventista ya Jengre, pamoja na wazazi na walezi wa wanafunzi.

Chuo cha Waadventista cha Sayansi za Uuguzi cha Jengre kilianzishwa ili kuendeleza wataalamu wa afya ambao ni hodari katika taaluma yao na wenye mizizi mizito katika maadili ya Kikristo. Taasisi hiyo inapoendelea kukua, inabaki kujitolea kuzalisha wauguzi ambao watafaulu si tu katika utaalam wa kimatibabu bali pia kuwa alama za huruma na uadilifu katika sekta ya huduma za afya.

Makala asili ilitolewa na Divisheni ya Afrika Magharibi na Kati.

Ezinwa Alozie, Konferensi ya Yunioni ya Kaskazini mwa Nigeria

Topics

  • Education
  • Healthcare
  • News

Related articles

Adventists keep assisting affected one month after Venezuela earthquakes

Adventists keep assisting affected one month after Venezuela earthquakes

August 15, 2026

Humanitarian

Andrews University hosts founding of NESTX

Andrews University hosts founding of NESTX

August 15, 2026

Education

Adventure Bible Game expands as Atlantic Union launches new pilot program for toddlers

Adventure Bible Game expands as Atlantic Union launches new pilot program for toddlers

August 14, 2026

Children

Building permit for local Adventist church in Bulgaria attained after 25 years of prayer

Building permit for local Adventist church in Bulgaria attained after 25 years of prayer

August 14, 2026

Human Interest

Subscribe for our weekly newsletter

Related Topics

More topics

Education

In the Solomon Islands, ADRA provides seeds to strengthen food security

In the Solomon Islands, ADRA provides seeds to strengthen food security

July 5, 2026
June 29, 2026

Adventist teacher faces long recovery after shark attack

June 15, 2026

Redevelopment Begins at Local Adventist Vocational School in the Solomon Islands

April 27, 2026

In Papua New Guinea, Adventist School Dedicates New Bus to Support Ministry and Staff

More from Education

Healthcare

Adventist Health foot care kits support wound care in Fiji

Adventist Health foot care kits support wound care in Fiji

August 13, 2026
August 2, 2026

Health team in the Solomon Islands delivers care behind prison walls

July 29, 2026

Free healthcare provided to communities in the Solomon Islands

July 16, 2026

Adventist health event offers hope for type 2 diabetes

More from Healthcare